Back

FUNGUA UBONGO -DENIS MPAGAZE

Sh5,000.00

Kwahiyo nimekuandikia kitabu hiki walau kikusaidie kufungua ubongo na kuanza kufikiri mambo makubwa kama wanavyofanya waliofanikiwa katika kila kitu. Donald Trump anasema, “Watu wengi hufikiria mambo madogo kwa sababu wanaogopa mafanikio makubwa.” Yeye anapenda kufikiri makubwa ndiyo maana anafahamika duniani kwa kumiliki majengo marefu sana. Kwa nini na sisi tusianze kufikiria mambo makubwa tukaachana na majungu? Basi tuanze leo kwa kusoma kitabu hiki!

-
+
Category:

Kama kuna zawadi kubwa aliyotupa Mungu basi ni ubongo. Kazi ya ubongo ni kufikiri, lakini cha kusikitisha kazi ya kufikiri tumewaachia watu wachache sana duniani. Wanaumizi vichwa kwa niaba yetu. James Madson anakwambia ni asilimia nne tu ya watu wote duniani ndio wanaofikiri, waliobaki wanaona ni bora wafe kuliko kufukiri. Wengi wamebaki kuwa washabiki na watumiaji wa kazi za wanaofikiri. Ikitokea wamefikiri basi wanafikiri vitu vidogo vidogooo! “Fulani anajifanya amesoma lakini hata haolewi”. “Ana umbo zuri lakini hajui kuvaa.” “Matajiri wote ni wezi na washirikina.”

Kwahiyo nimekuandikia kitabu hiki walau kikusaidie kufungua ubongo na kuanza kufikiri mambo makubwa kama wanavyofanya waliofanikiwa katika kila kitu. Donald Trump anasema, “Watu wengi hufikiria mambo madogo kwa sababu wanaogopa mafanikio makubwa.” Yeye anapenda kufikiri makubwa ndiyo maana anafahamika duniani kwa kumiliki majengo marefu sana. Kwa nini na sisi tusianze kufikiria mambo makubwa tukaachana na majungu? Basi tuanze leo kwa kusoma kitabu hiki!

Reviews

There are no reviews yet.

Be the first to review “FUNGUA UBONGO -DENIS MPAGAZE”

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!